Mafunzo juu ya sera na sheria za ardhi yametolewa kwa wakulima wawezeshaji (mapromota) 30 ambao ni wanachama wa MVIWATA mkoani Mbeya. Mafunzo hayo yamejumuisha wakulima kutoka Wilaya za Mbarali, Momba na Mbozi. Mafunzo yamefanyika kwa muda wa wiki 2 katika Chuo cha Kilimo Uyole Jijini Mbeya.





