SHIRIKA LA MAENDELEO LA USWISI (SDC) LATEMBELEA VIKUNDI VYA WAKULIMA WADOGO

Ugeni kutoka shirikia la maendeleo la Uswisi (SDC) umetembelea vikundi vya wakulima wadogo ambao ni wanachama wa Mtandao wa Vikundi vya Wakulima Tanzania (MVIWATA) katika wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro. Lengo la ugeni huu ni kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na MVIWATA. Ugeni huo ulitembelea  vijiji vya Maduhu, Mvumi na Rudewa Gongoni.

Wageni walijionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na wakulima wadogo kupitia MVIWATA. Wanachama walieleza namna MVIWATA ilivyowasaidia kwa kuwapa mafunzo mbalimbali kama vicoba, ujasiriamali, sheria za ardhi, haki za watoto na wanawake na kilimo cha umwagiliaji. Mafunzo ambayo yamewajengea uwezo na yamewasaidia kujikwamua kiuchumi, ambapo wameitaka MVIWATA kuendelea kutoa mafunzo ili yawasaidie zaidi.

Wageni wamefurahishwa na namna ambavyo MVIWATA inafanya kazi zake kwa kutetea maslahi ya wakulima wadogo kwa kuhakikisha kwamba mkulima mdogo ana nufaika.

Mviwata on Facebook

Subscribe to our monthly newsletter