WANACHAMA WA MVIWATA WAANZISHA SACCOS.

Wanachama wa MVIWATA kata ya Magungu wilaya Kiteto mkoani Manyara wameanzisha SACCOS ili kuweza kupata huduma za kifedha. SACCOS hiyo ijulikanayo kama MANGE SACCOS ni muunganiko wa vijiji vitatu Magungu, Nhati na Emarti. SACCOS hiyo imeanzishwa kutokana na uhamasishaji uliofanywa na wananchama kwa kushirikiana na viongozi wa mitandao ya msingi Magungu na Nhati.

Wanachama hawa wa MVIWATA waliamua kuanzisha SACCOS kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa mitaji, umbali wa huduma za kifedha na mikopo ya mabenki yenye riba kubwa. Wanachama hawa wameanzisha SACCOS ili kukuza uchumi na kupunguza umaskini, SACCOS hii itawawezesha wanachama  kuweza kukopa kwa malengo ili kuendesha shughuli zao mbalimbali ikiwemo kilimo na biashara. Kwasasa SACCOS hiyo ina wanachama 70, wanaume 40 na wanawake 30. Mange SACCOS ina mpango wa kufikia wananchama 200 kwa kipindi cha miaka miwili.

Aidha wanachama hao wameshukuru shirika la MVIWATA kwa mchango wake kwa kusaidia katika hatua ya uanzishwaji wa SACCOS ambapo shirika liligharimia wanachama 8 kwenda ziara ya mafunzo  kuhusu SACCOS. Wanachama hao wa MVIWATA walienda katika SACCOS 2 zilizopo mkoani Morogoro, Kinole SACCOS  na Mkuyuni SACCOS. Katika ziara hii ya mafunzo waliweza kujifunza mengi ikiwemo uendeshaji, mafanikio pamoja na changamoto.

SACCOS nyingi zinazoanzisha huwa zinachangamoto kubwa sana na saa nyingine hupelekea kufa kabisa sababu hizi ni kama ukosefu wa uaminifu kwa wanachama wenyewe, ukosefu wa uaminifu kwa wasimamizi na watendaji wa SACCOS kutokuwa na elimu ya kutosha. Suala hili Mange SACCOS wamelitafakari kwa kina na kukubali kuwa watakabiliana na changamoto hizi, wakiifuata kauli mbiu yao isemayo “hakuna kushindwa tukiwa waaminifu, SACCOs ni chombio cha huduma sio chombo cha huruma”.

 

Mviwata on Facebook

Subscribe to our monthly newsletter